MFANO WA BARUA YA MAAFISA UTAMADUNI
Je, unatafuta nafasi ya kazi kama Afisa Utamaduni Daraja la II? Barua hii ya maombi ni mfano mzuri wa jinsi ya kuandaa maombi yako ili kujitokeza kwa waajiri. Itakusaidia kueleza sifa zako na utayari wako kwa ufanisi.
KABLA YA KUPAKIA BARUA HAKIKISHA
Umepiga Mihuri ya Mwanasheria kwenye Documents zako
Umewaweka wadhamini wako watatu na kuendelea wa kuaminika
Umeweka Passport size yako yenye Background ya Blue
Umebadilisha Makazi yako ya kudumu na kuweka unayoishi sasa kwani (ndiyo wanatumia kupanga eneo la Interview)
KARIBU
AFISA UTAMADUNI MTARAJIWA,
S.L.P 259,
DODOMA.
4/8/2024
KATIBU,
OFISI YA
RAIS,
SEKRETARIETI
YA AJIRA KATIKA UTUMISHI WA UMMA,
S. L. P.
2320,
DODOMA.
Ndugu,
YAH: MAOMBI YA KAZI YA AFISA
UTAMADUNI DARAJA LA II (CULTURAL OFFICER II)
Husika na kichwa cha habari hapo juu,
Mimi
ni kijana wa kitanzania mwenye umri wa miaka 26, nimehitimu Shahada ya Awali ya
Fasihi ya Kiswahili kutoka chuo kikuu cha Dodoma. Kutokana na tangazo la nafasi
za kazi zilizotangazwa tarehe 3 Agosti 2024 ninaomba nafasi ya kazi ya Afisa Utamaduni Daraja la II (Cultural
Officer II).
Nina
uzoefu katika shughuli za utamaduni, na ninauwezo wa kufanya kazi kwa ufanisi
na weledi. Nimejihusisha na shughuli za kiutamaduni kwa kufanya kazi kama Afisa
utamaduni kipindi cha mafunzo kwa vitendo, ambazo zimenipa ujuzi na mbinu za
kusaidia jamii kwa ufanisi.
Ninaahidi kuifanya
kazi kwa uaminifu na ufanisi kwa maendeleo ya nchi na Taifa kwa ujumla pia nipo
tayari kufika kwenye usaili wakati wowote nitakapohitajika ili kutoa maelezo
zaidi kuhusu ujuzi na uzoefu wangu
Naambatanisha na
vyeti vyangu vya taaluma ikiwemo na wasifu wangu binafsi.
Wako
katika ujenzi wa taifa
………………………
AFISA UTAMADUNI MTARAJIWA
0712345678
Kwa msaada wa kufanyiwa kazi ajira portal, tafadhali wasiliana nami kwa namba 0659385219. Namba hii pia inapatikana kwenye WhatsApp: Bonyeza hapa kuwasiliana nami.
kuingia ajira portal 👉 https://portal.ajira.go.tz/home
.jpeg)



